Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini

Share

Ukurasa rasmi ya Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda mjini- Kituo cha cha taarifa ,huduma na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

02/06/2026

NJIANI KUELEKEA MOROCCO

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, akiwa pamoja na Mhe.Haji Manara ndani ya ndege kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya kutoa hamasa kwa timu ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, ambayo itashuka dimbani kesho kucheza mchezo wa fainali.

Mhe. Bulaya ni miongoni mwa wabunge waliochaguliwa kuiunga mkono na kuitia moyo timu ya Serengeti Boys katika fainali itakayozikutanisha Tanzania na Senegal, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha vijana wetu kufanya vizuri na kuendelea kuipeperusha vyema bendera ya taifa katika mashindano hayo.

Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini inawatakia kila la heri Serengeti Boys katika mchezo huo muhimu wa fainali.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

01/06/2026

HONGERA SANA MHE. ESTER AMOS BULAYA

HAKIKA WANABUNDA MJINI WANAJIVUNIA UTENDAJI KAZI WAKO

Photos from Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini's post 01/06/2026

Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini Mhe. Ester Bulaya ametoa vifaa vya michezo kwa timu ya Bajaji FC, lakini pia ametoa vifaa vya ofisi kwaajili ya kuendeshea Umoja wa Madereva Bajaji Mji wa Bunda

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

30/05/2026

MASJIDI NURU - MIGUNGANI

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, ametoa sadaka ya vitabu vya dini vya Qur'an na Juzuu katika Msikiti wa Nuru uliopo Mtaa wa Migungani, Kata ya Bunda Stoo.

Sadaka hiyo imelenga kuunga mkono shughuli za kiibada na kuwasaidia waumini wa msikiti huo katika kujifunza na kusoma Qur'an. Katibu wa Mbunge kwa niaba ya Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushikamana na maadili ya dini pamoja na kuimarisha elimu ya kiroho katika jamii.

Kiongozi wa Msikiti wa Nuru(MASJIDI NURU) alimshukuru Mbunge kwa msaada huo, alielezea kuwa vitabu hivyo vitakuwa na manufaa makubwa kwa watoto, vijana na waumini wote wanaoshiriki masomo ya dini katika msikiti huo.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

30/05/2026

BUNDA MJINI – MARA

Wanafunzi wa Madrasa katika Masjid Nuru iliyopo Mtaa wa Migungani, Kata ya Bunda Stoo, Wilaya ya Bunda, wamemsomea dua Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe.Ester Amos Bulaya, kufuatia msaada wake wa kutoa vitabu vya dini ikiwemo Qur'an na Juzuu kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi hao katika masomo yao ya dini.

Dua hiyo ilisomwa mara baada ya kukabidhi vitabu hivyo katika msikiti huo, ambapo wanafunzi pamoja na walimu wao walimshukuru kwa moyo wa kujitolea na mchango wake katika kuendeleza elimu ya dini kwa watoto na vijana.

Katibu wa Mbunge aliwashukuru viongozi wa dini, walimu wa madrasa na wanafunzi kwa dua hiyo, akisisitiza umuhimu wa elimu ya dini katika kujenga maadili mema, amani na mshikamano ndani ya jamii.

Tukio hilo limepokelewa kwa furaha na waumini pamoja na wananchi wa Msikiti huo, huku likionyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya viongozi na jamii katika kuendeleza ustawi wa wananchi.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini.

28/05/2026

ESTER BULAYA AWAAGA VIJANA WA UMITASHUMTA WANAOENDA TARIME KUIWAKILISHA BUNDA MJINI

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, kupitia Katibu wa Mbunge, M***a Hussen, kwa kushirikiana na viongozi wa CCM, leo wamewatembelea na kuwaaga vijana wa UMITASHUMTA walioteuliwa kwenda kuiwakilisha Halmashauri ya Mji wa Bunda katika mashindano ya kimkoa yanayofanyika Halmashauri ya Tarime.

Akizungumza na vijana hao kabla ya safari yao, Katibu wa Mbunge, M***a Hussen, aliwataka kwenda kuitendea haki Halmashauri ya Mji wa Bunda pamoja na Jimbo la Bunda Mjini kwa kuonyesha nidhamu, kujituma na ushindani wa hali ya juu katika mashindano hayo.

Aidha, aliwahimiza kuwa mabalozi wazuri wa Bunda kwa kudumisha umoja, mshikamano na uzalendo wakati wote wa mashindano.

M***a Hussen pia alikumbusha kuwa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Ester Bulaya, hivi karibuni alitoa vifaa vya michezo kwa makundi yote ya vijana wanaoshiriki mashindano hayo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha michezo na kuendelea kukuza vipaji vya vijana ndani ya halmashauri hiyo.

Kwa upande wao, viongozi walioambatana na ujumbe huo waliwatakia vijana hao safari njema pamoja na mafanikio mema katika mashindano hayo ya kimkoa yanayofanyika Tarime.

27/05/2026
26/05/2026

Tarehe: 26 Mei, 2026

BUNGE LA KUMI NA TATU (13)
Mkutano wa Tatu – Kikao cha Thelathini na Saba (37)

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, ameuliza maswali bungeni akitaka kufahamu:-

1. Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya ucheleweshwaji wa upatikanaji wa chakula katika miradi ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba, hali inayosababisha wafugaji kupata hasara kubwa pamoja na kuhatarisha ukuaji na uhai wa samaki?

2. Ni lini Serikali itawapatia vijana walioomba boti za kisasa kwa ajili ya shughuli za uvuvi, hususan vijana wa Jimbo la Bunda Mjini, ili waweze kufanya uvuvi wa kisasa na kujiongezea kipato?

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

26/05/2026

Tarehe: 26 Mei, 2026

BUNGE LA KUMI NA TATU (13)
Mkutano wa Tatu – Kikao cha Thelathini na Saba (37)

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, ameuliza swali bungeni akitaka kufahamu ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

26/05/2026

Tarehe: 25 Mei, 2026

BUNGE LA KUMI NA TATU (13)
Mkutano wa Tatu – Kikao cha Thelathini na Sita (36)

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, ameuliza swali bungeni akitaka kufahamu chanzo cha kukatika kwa huduma ya maji katika Jimbo la Bunda Mjini kwa zaidi ya wiki tatu, hali inayosababisha kero kubwa kwa wananchi wa jimbo la Bunda Mjini.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

Want your business to be the top-listed Government Service in Bunda?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address

250
Bunda
818196