31/10/2024
Mechi ya watani wa jadi kutoka Soko la Kimataifa la Samaki ( Feri ) imelizika kwa Umoja Fc kuifunga timu ya Kijiwe Sugu Fc bao Moja kwa bila na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali kwenye michuano ya mchezo wa beach soka katika Mashindano ya kombe la Mama Samia Ferry Fish Market.
Mashindano haya yaliyoandaliwa na Uongozi wa Soko Chini ya Meneja wa soko Ndg. Suleman Mfinanga na Mwenyekiti wa wadau Ndg. Mbaraka Kilima.
Akizungumza kocha wa timu ya Umoja Bw. Ronaldo mara baada ya kumalizika mechi amesema , "ushindi huu tuliutegemea kwasababu tulijiandaa vya kutosha kwenye uwanja wa mazoezi na wachezaji wangu wamefanya vizuri licha kupata kadi nyekundu moja ."
Naye Kapteni wa timu ya Umoja Fc Mohamed Hafidh amesema , "tumepata ushindi kwasababu tumefuata maelekezo ya kocha wetu japo kuwa watani wetu walikuwa wagumu lakini tunashukuru tumefanya vizuri na kufanikiwa kutinga hatua inayofuata . "
Mdau wa michezo kutoka Feri Bw. Athumani sanga amesema kuwa wanamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika mashindano haya kwasababu licha ya zawadi mbali mbali zinazoshindaniwa lakini pia michezo inaleta watu pamoja na kudumisha tamaduni ya kufanya mazoezi.
Mashindano haya bado yapo katika hatua ya makundi huku baadhi ya timu zikiwa zimefuzu hatua ya robo fainali.

16/01/2022
28/12/2021