13/05/2026
VIONGOZI WA WIZARA, TAMISEMI NA BMT WAKUTANA NA KATIBU TAWALA MKOA WA MANYARA
Viongozi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), leo Mei 13, 2026 wamekutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Bi. Maryam Mhaji kwa lengo la kujitambulisha rasmi ofisini hapo.
Katika kikao hicho, Bi. Mhaji ameushukuru uongozi wa wizara pamoja na BMT kwa kuupa Mkoa wa Manyara kipaumbele katika maendeleo ya michezo, hususan kupitia mafunzo ya walimu wa michezo yanayoendelea mkoani humo.
Amesema mafunzo hayo yanayowakutanisha walimu wa michezo kutoka mikoa ya Manyara na Arusha yataongeza ujuzi na uwezo wa walimu katika kuibua na kuendeleza vipaji vya wanafunzi mashuleni.
Aidha, ameeleza kuwa Mkoa wa Manyara utaendelea kushirikiana na wadau wa michezo kuhakikisha michezo inakuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya vijana na jamii kwa ujumla.
12/05/2026
MAFUNZO YA WALIMU WA MICHEZO KUTOKA MIKOA YA ARUSHA NA MANYARA
12/05/2026
MAFUNZO YA WALIMU WA MICHEZO KWA WATU WENYE ULEMAVU ( IRINGA)
12/05/2026
MAKONDA ASAINI HATI YA MAKUBALIANO UENDESHAJI AFCON 2027 – MOTSEPE ASHUHUDIA
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda (Mb), leo amesaini hati ya makubaliano ya uendeshaji wa mashindano ya AFCON 2027, inayojulikana k**a CAF Joint Resolution Total Energies.
Tukio hilo la kihistoria limeshuhudiwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, jijini Nairobi, nchini Kenya.
Hatua hiyo inalenga kuimarisha uratibu na ushirikiano katika maandalizi ya mashindano makubwa ya soka barani Afrika.
Aidha, katika mazungumzo hayo, wamejadili hatua muhimu kuelekea mashindano ya AFCON 2027, ikiwamo tathmini ya hatua iliyofikiwa na nchi katika maandalizi, utayari wa kitaifa, pamoja na maendeleo ya miundombinu inayohitajika.
Vilevile, Serikali imewasilisha ombi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kutumia lugha ya Kiswahili k**a lugha rasmi katika mashindano hayo ya mwaka 2027.
Mkutano huo ulijumuisha mawaziri kutoka nchi tatu wenyeji wa AFCON 2027, Kenya, Uganda na Tanzania, pamoja na wenyeviti wa k**ati za maandalizi za AFCON (LOC), Marais wa mashirikisho ya mpira wa miguu ya nchi hizo, pamoja na wataalamu wengine kutoka wizara za michezo katika nchi waandaaji.
09/05/2026
Maandalizi yamepamba moto ndani ya Ukumbi wa The Super Dome Masaki tayari kwa usiku mkubwa wa Tuzo za BMT leo Mei 09, 2026
Mandhari, mwanga na mpangilio vinaonyesha wazi kuwa usiku wa leo utakuwa wa kipekee kwa wanamichezo na wageni wote watakaohudhuria.
07/05/2026
WANAOWANIA TUZO KIPENGELE CHA WANAHABARI BORA WA KIUME WA MWAKA 2025
07/05/2026
WANAOWANIA TUZO KIPENGELE CHA MWANAHABARI BORA WA K**E WA MWAKA 2025