Ushetudc

Ushetudc

Share

UKURASA RASMI WA FACEBOOK WA HALMASHAURI YA WILAYA YA USHETU

Photos from Ushetudc's post 18/07/2026

WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI USHETU,WAPONGEZWA,WAPANGA MIKAKATI YA KUONDOA ZERO KATIKA MITIHANI YA TAIFA

USHETU DC
JULAI 18,2026

Walimu wote wa shule za sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu leo wamekutana katika kikao maalum cha kutoa pongezi kwa shule na walimu waliofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa, sambamba na kuweka mikakati mipya ya kuendelea kuinua kiwango cha elimu ndani ya halmashauri.

Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Amali Nyamilangano kiliongozwa na Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Pia kilihudhuriwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Bi. Hadija Kabojela, Afisa Elimu wa Mkoa, Afisa Elimu wa Halmashauri pamoja na viongozi na wadau mbalimbali wa elimu.

Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kuwapongeza walimu na shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya Kidato cha Pili, Kidato cha Nne na Kidato cha Sita, pamoja na kujadili mikakati itakayosaidia kuongeza ufaulu na kuboresha zaidi sekta ya elimu katika shule zote za sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Bi. Hadija Kabojela, alisema halmashauri imejipanga kuhakikisha inaondoa kabisa matokeo ya sifuri (Zero) katika shule zote za sekondari. Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya walimu, viongozi wa shule na kubadilishana uzoefu kati ya shule ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mhe. Emmanuel Cherehani, alisema Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa kusambaza huduma ya umeme katika taasisi za umma, ikiwemo shule. Alieleza kuwa hadi sasa zimebaki shule nne pekee ndani ya Halmashauri ambazo bado hazijapatiwa umeme.

Katika kikao hicho, Meneja wa TANESCO aliyeshiriki aliwahakikishia washiriki kuwa Serikali tayari imeshatenga fedha kwa ajili ya kupeleka umeme katika shule tatu kati ya hizo, huku akiahidi kuwasilisha maombi ili shule moja iliyobaki nayo ipatiwe huduma hiyo.

Kikao kilihitimishwa kwa zoezi la utoaji wa vyeti na zawadi kwa walimu pamoja na shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa ya mwaka 2025 na 2026, ikiwa ni sehemu ya kutambua juhudi zao na kuhamasisha ari ya kufanya vizuri zaidi.

Photos from Ushetudc's post 18/07/2026

KAMATI YA MKOA YA URATIBU WA MWENGE WA UHURU 2026 YAKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU USHETU

USHETU DC
JULAI 18,2026

Kamati ya Mkoa ya Uratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, tarehe 17 Julai 2026, ilifanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu kwa lengo la kukagua na kutathmini miradi mbalimbali ya maendeleo inayotarajiwa kupitiwa, kuzinduliwa na kuwekwa jiwe la msingi na Mwenge wa Uhuru mwaka 2026.

Katika ziara hiyo, k**ati ilitembelea miradi kutoka sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, maji, mazingira na miundombinu. Lengo la ukaguzi huo lilikuwa ni kujiridhisha kuhusu ubora wa utekelezaji wa miradi hiyo, maendeleo yaliyofikiwa pamoja na utayari wake kwa ajili ya kupokelewa na Mwenge wa Uhuru.

Aidha, Kamati ilitoa maelekezo na ushauri katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa viwango vinavyokubalika na kutoa huduma bora kwa wananchi, sambamba na kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Photos from Ushetudc's post 17/07/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ushetu anaipongeza Idara ya Uvuvi kwa uratibu mzuri wa zoezi hili lililowezesha watumishi kupata samaki wenye ubora kwa bei nafuu, na inaendelea kuwahamasisha wadau kuandaa fursa k**a hizi zenye manufaa kwa watumishi na jamii kwa ujumla.


Cc Hadija Mohamed Kabojela ✍🏿

17/07/2026

Lydia Felix Kaena
Afisa Maendeleo ya Jamii


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania

17/07/2026

“Tule Samaki kwa ajili ya Afya bora, tuongeze ubora wa ubongo wetu”
Frida Izrael - Afisa Uvuvi | Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania

17/07/2026

Deus Kakulima Antony
Mkuu wa Div. Kilimo | Mifugo na Uvuvi


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania Wizara ya Mifugo na Uvuvi Wizara ya Kilimo

Photos from Ushetudc's post 17/07/2026

UUZAJI WA SAMAKI WAFANA KWA KIWANGO KIKUBWA HALMASHAURI YA USHETU

Uuzaji wa samaki uliofanyika leo katika jengo la zamani la Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu umefanyika kwa mafanikio makubwa, huku watumishi wengi wakijitokeza kununua samaki bora kwa bei nafuu.

Samaki hao waliuzwa kwa bei ya Shilingi 10,000 kwa kilo, ambapo mwitikio mkubwa wa watumishi umeonesha kuridhishwa na ubora wa samaki pamoja na bei iliyotolewa.

Halmashauri inawashukuru watumishi wote waliojitokeza kushiriki katika zoezi hilo na itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuleta fursa k**a hizi kwa manufaa ya watumishi na jamii kwa ujumla.


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania

17/07/2026

“Tunajivunia kuwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu. Sisi k**a kikundi tumekuweka kuwa mlezi wetu”
Cc Hadija Mohamed Kabojela

17/07/2026

“Mafunzo ya ubanguaji korosho yameambatana na ugawaji wa viuatilifu”

Mapenzi Wilson Mshana.
Afisa Kilimo - H.W Ushetu


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania Wizara ya Kilimo

17/07/2026

Faustine Samwel Kayungilo
Afisa kilimo - Bodi ya korosho


Mboni Mimi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama FRANK NKINDA 🇹🇿 Hadija Mohamed Kabojela Emmanuel Peter Cherehani Maelezo News Goldfm Tanzania

Want your business to be the top-listed Government Service in Kahama?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address

Kahama