Wanafunzi wa Kidato Shule ya Sekondari Gungu ilipokea kiasi cha Million 220, kwa Ujenzi wa Vyumba 11, Angalia Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza Walivyoishukuru Serikali kwa Miundombinu iliyopo Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Mawasiliano Ofisi ya Rais - Tamisemi
Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji, Government Organization, P. O. BOX 44, Kigoma.
05/01/2023
UPASUAJI WA KWANZA KITUO CHA AFYA CHA GUNGU MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI WAFANYIKA
Posted On: January 5th, 2023
Na Mwandishi Wetu
Upasuaji wa kwanza kwa Mama mjamzito katika kituo cha afya cha Gungu umefanyika Leo January 5, 2023 Mara baada ya uzinduzi wa kuanza kwa huduma hiyo
Upasuaji huo umeanza Mara baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. kuzindua kuanza rasmi kwa huduma hiyo ya Upasuaji katika kituo hicho cha Afya cha Gungu
Akizindua huduma hiyo Mkuu huyo wa Wilaya ameipongeza na kushukuru Serikali kwa namna ambavyo imeendelea kuboresha huduma za afya katika Wilaya hiyo ikiwemo uboreshaji wa huduma na Ujenzi wa Majengo katika Kituo cha afya kipya cha Buhanda na uboreshaji wa huduma kituo cha afya cha Ujiji
Aidha amewataka Watumishi wa Afya kufanya kazi kwa weredi na kuonesha upendo kwa Wagonjwa wanaofika kupata huduma ya matibabu katika kituo hicho wakiwemo Wajawazito watakaokuwa wakipata huduma ya upasuaji mara baada ya uchungu pingamizi katika kipindi cha kujifungua
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Dr. amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr. imefanikisha Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje, Maabara, Jengo la kufulia, jengo la wodi ya Wazazi na Upasuaji katika kituo hicho cha afya cha Gungu kwa gharama ya fedha za Kitanzania Millioni Mia tano (Tsh 500, 000, 000/=) ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa vya Upasuaji pamoja na vifaa vya uhifadhi damu salama
Amesema Serikali imeendelea kufanya uboreshaji wa huduma katika kituo hicho ikiwa ni pamoja na kuongeza damu kutokana na uwepo wa vifaa vya utunzaji damu salama
Amesema kupatikana kwa huduma hizo kutaondoa utoaji rufaa kwa Wagonjwa kuelekea katika hospitali ya Babtisti na Hospitali ya rufaa ya Maweni kupata huduma ya Upasuaji pamoja na kuongezewa damu
Nao baadhi ya Wananchi Waliohudhuria katika ufunguzi huo akiwemo Samsoni Nathani na Bi. Grace Nashoni wameipongeza Serikali kwa jitihada za uboreshaji na upatikanaji wa huduma bora za afya huku wakisema huduma hizo utahakikisha Usalama wa maisha ya Mama na Mtoto pindi Mjamzito anapojifungua
24/12/2022
WATAALAMU WAAHIDI KUSIMAMIA KIKAMILIFU MRADI MPYA WA BOOST
Posted On: December 24th, 2022
Na Mwandishi Wetu
Wataalamu wa Halmashauri na Mikoa ya Kigoma na Kagera wameahidi kutekeleza mradi wa BOOST kikamilifu Ili kuleta ufanisi na matokeo yaliyokusudiwa
Wameyasema hayo Mapema Jana Desemba 23, 2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili (02) yaliyokuwa na lengo la kuzijengea timu za utekelezaji wa mradi huo wa BOOST
Akizungumza katika katika mafunzo hayo kwa niaba ya Wahandisi wengine Mhandisi wa Ujenzi Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Joel Shirima alisema katika Mradi wa BOOST ambao utahusisha Ujenzi wa Miundombinu ya Madarasa watahakikisha wanasimamia kikamilifu katika kutoa Ushauri wa Kitaalamu na Kiutendaji
Naye Afisa Mipango, Uchumi na Mipango kutoka Halmashauri ya Biharamuro Mkoani Kagera Ndugu. Jasphone issanzu Mkurugu alisema Halmashauri zipo tayari katika kupanga bajeti za utekelezaji kikamilifu kwa kushirikiana na idara mbalimbali na kuhusisha mapato ya Ndani na ushirikishaji wa Jamii
Awali akihutubia washiriki hao kabla ya kufunga mafunzo hayo Katibu Tawala Msaidizi idara ya elimu Mkoa wa Kigoma Bi. Paulina NdigezĂ aliwataka Wataalamu hao kutekeleza kikamilifu afua mbalimbali zilizofundishwa
Mradi wa BOOST unatarajiwa kutekelezwa kwa mda wa miaka mitano (05) kwa Mwaka 2021/2022 hadi Mwaka 2025/2026 kwa fedha za Kitanzania Trillion 1. 15 sawa na Dola za Kimarekani Million Mia tano (500)
Katika fedha hizo Dola za Kimarekani Million 480 zitatumika katika program ya lipa kulingana na matokeo na Dola za Kimarekani Million 20 ni gharama za utekelezaji wa uwekezaji wa miradi
Jumla ya vyumba vya Madarasa 12, 0000 vinatarajia kujengwa, ununuzi wa vifaa vya kisasa vya Tehama kwenye Shule zaidi ya mia nane (800) za Msingi na Vituo vya Walimu, na uandaaji wa vifaa vya kufundishia na Kujifunzia kwa elimu ya awali
Wataalamu Waliohudhuria mafunzo hayo ni pamoja na Maafisa elimu, Walimu wakuu, Waratibu elimu Kata, Wahandisi, Maafisa Maendeleo ya jamii, Maafisa Ustawi wa Jamii, Wahasibu, Maafisa mipango na Uchumi, Maafisa Manunuzi, Wadhibiti ubora wa elimu pamoja na Maafisa Mawasiliano Serikalini
22/12/2022
Baadhi ya Washiriki waliohudhuria mafunzo ya siku mbili (02) ya mradi mpya wa BOOST yaliyoanza leo Desemba 22, 2022 yakihusisha Wataalamu mbalimbali kutoka ngazi za Mkoa na Halmashauri kutoka Mikoa ya Kigoma na Kagera katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu kwa lengo la kuzijengea timu za utekelezaji wa mradi huo
Wataalamu hao Waliohudhuria mafunzo hayo ni pamoja na Maafisa elimu, Walimu wakuu, Waratibu elimu Kata, Wahandisi, Maafisa Maendeleo ya jamii, Wahasibu, Maafisa mipango na Uchumi, Maafisa Manunuzi, Wadhibiti ubora wa elimu pamoja na Maafisa Mawasiliano Serikalini
22/12/2022
NAMNA MRADI WA BOOST UTAKAVYOINUFAISHA JAMII KATIKA MASUALA YA ELIMU NCHINI
Posted On: December 22nd, 2022
Na Mwandishi Wetu
Wataalamu mbalimbali kutoka ngazi za Mkoa na Halmashauri kutoka Mikoa ya Kigoma na Kagera Leo Desemba 22, 2022 Wamekutana katika mafunzo ya siku mbili (02) katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kasulu kwa lengo la kuzijengea timu za utekelezaji wa mradi mpya wa BOOST
Wataalamu hao Waliohudhuria mafunzo hayo ni pamoja na Maafisa elimu, Walimu wakuu, Waratibu elimu Kata, Wahandisi, Maafisa Maendeleo ya jamii, Wahasibu, Maafisa mipango na Uchumi, Maafisa Manunuzi, Wadhibiti ubora wa elimu pamoja na Maafisa Mawasiliano Serikalini
Mgeni rasmi wa Mafunzo hayo ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi idara ya elimu Mkoa wa Kigoma Bi. Paulina NdigezĂ akihutubia Washiriki wa mafunzo hayo amewataka kuzingatia mafunzo hayo kwa lengo la kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa ufanisi
Awali Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka OR-TAMISEMI Ndugu. George Jackson Mbijima amesema mradi wa BOOST unatarajiwa kutekelezwa kwa mda wa miaka mitano (05) kwa Mwaka 2021/2022 hadi Mwaka 2025/2026 kwa fedha za Kitanzania Trillion 1. 15 sawa na Dora za Kimarekani Million Mia tano
Amesema katika fedha hizo Dola za Kimarekani Million 480 zitatumika katika program ya lipa kulingana na matokeo na Dola za Kimarekani Million 20 ni gharama za utekelezaji wa uwekezaji wa miradi
Ameendelea kusema katika Mradi huo jumla ya vyumba vya Madarasa 12, 0000 vinatarajia kujengwa, ununuzi wa vifaa vya kisasa vya Tehama kwenye Shule zaidi ya mia nane (800) za Msingi na Vituo vya Walimu, na uandaaji wa vifaa vya kufundishia na Kujifunzia kwa elimu ya awali
Aidha malengo mengine ya mradi ni kuongeza uandikishaji wa elimu ya awali kutoka 76.9% mwaka 2021 hadi zaidi ya 85%, mafunzo endelevu ya Walimu kazini (MEWAKA), na Halmashauri kusimamia utawala bora katika elimu kwa kuzingatia miongozo na usimamizi wa Shule
Amehitimisha kwa kusema Shule za Msingi 6,000 zitateleleza mradi wa programu ya Shule ya Msingi Salama na kufanya Wanafunzi 50% wa darasa la pili kufikia kiwango cha chini cha kumudu stadi za Kusoma na kuandika na 35% katika kuhesabu
Mradi wa BOOST tayari Umeanza kutekelezwa Nchini Tanzania kwa Mikoa ya Tanzania bara kwa kutoa mafunzo mbalimbali na utambulishaji wa mradi na unatarajia kuboresha upatikanaji wa fursa sawa katika ujifunzaji bora wa Elimu Ofisi ya Rais - Tamisemi Msemaji Mkuu wa Serikali Ikulu Mawasiliano
21/12/2022
CCM WILAYA YA KIGOMA YARIDHISHWA NA UJENZI WA VYUMBA MADARASA KIGOMA/UJIJI
Posted On: December 21st, 2022
Na Mwandishi Wetu
Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigoma Jana Desemba 20, 2022 walifanya ziara ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa 57 unaoendelea Manispaa ya Kigoma/Ujiji ikiwa ni ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya chama hicho
Katika ziara hiyo Viongozi na Wajumbe wa Kamati hiyo waliridhishwa na ujenzi huku wakipongeza usimamizi wa Wataalamu chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo
Manispaa hiyo ilipokea kiasi cha fedha za Kitanzania Billion moja na milion mia moja arobaini na Sita (Tsh 1, 146, 000, 000/=) kutoka Serikali Kuu kwa lengo la ujenzi wa vyumba hivyo vya Madarasa ikiwa ni maandalizi na mapokezi ya Wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa Mwaka 2023
Akizungumza Katika ziara hiyo Katibu wa itikadi uenezi wa CCM Wilaya ya Kigoma Ndugu. Haruna Kambiro aliwapongeza Wataalamu wa Manispaa hiyo kwa Usimamizi wa ujenzi wa Madarasa kwa Shule kumi na sita (16) huku akiwataka kuendelea kukamilisha ili kuwanufaisha wanafunzi pindi Shule zitakapofunguliwa
Mjumbe wa Kamati hiyo na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Kilumbe Shabani Ng'enda alisema ujenzi wa miundombinu hiyo unaendelea kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya Madarasa katika Manispaa hiyo na kufanya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya upili kuanza kwa wakati mmoja
Mjumbe wa Kamati hiyo na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe aliwataka Wananchi kuitunza Miundombinu hiyo kwa kutoruhusu uhalibifu wowote huku akiwataka Wazazi kuhakikisha kila Mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga na masomo ya upili anaripoti kwa wakati
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Athumani Msabila alisema ujenzi wa vyumba vya Madarasa unaendelea kukamilishwa katika hatua za mwisho ili kuanza kutumika mapema mwezi Januari 2023
Alihitimisha kwa kusema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali na inatarajia kuleta fedha zingine za Maendeleo katika Ujenzi wa Miundombinu ya vyumba vya Madarasa kwa Shule za Msingi kupitia mradi wa Boost
14/12/2022
"WALIMU ZINGATIENI MAFUNZO " Bi. PANGANI MRATIBU MSAIDIZI WA MRADI WA SHULE BORA
Posted On: December 14th, 2022
Na Mwandishi Wetu
Mratibu Msaidizi wa Mradi wa Shule Bora OR- TAMISEMI Bi. Adelaida Pangani amewataka walimu kuzingatia mafunzo yenye lengo la kuinua ubora wa elimu Nchini
Aliyasema hayo Jana Desemba 13, 2022 katika Mafunzo ya siku mbili (02) ya Walimu Kazini (MEWAKA) yanayoendelea katika Shule ya Msingi Kigoma yakihusisha Watendaji Kata, Waratibu Elimu Kata, Walimu Wakuu, Walimu Wataaluma na Walimu Mahili wa Shule za Msingi zilizopo Kata za Kigoma na Bangwe
Alisema lengo la Mafunzo hayo ni kuwawezesha Walimu kuibua hadithi za mafanikio za kujifunza za mfano zinazopatikana miongoni mwao ili kutatatua changamoto za ujifunzaji na ufundishaji ili kuinua ubora wa elimu nchini
Aliwataka Wasimamizi wa elimu ngazi za Kata kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa kuwashirikisha Wazazi na wadau mbalimbali wa elimu katika kukuza elimu Nchini
Mradi wa Shule bora umelenga kuinua kiwango cha elimu jumuishi pamoja na kuweka mazingira salama ya kujifunzia kwa Wanafunzi wote wa k**e na wa kiume katika Shule za Serikali za Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UK aid , gharama za mradi zikiwa ni Shilingi za Kitanzania bilion 271 na utafanya katika ngazi zote za mradi katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Rukwa, Singida, Dodoma, Simiyu, Mara, Tanga na Pwani ambapo utafikia kikomo mwaka 2027
12/12/2022
MAFUNZO YA WALIMU NA WASIMAMIZI WA ELIMU MRADI WA SHULE BORA
Posted On: December 12th, 2022
Na Mwandishi Wetu
Walimu na wasimamizi wa elimu ngazi ya kata jana Desemba 11, 2022 walihitimisha mafunzo ya siku mbili (2) yaliyokuwa na lengo la kuwawezesha walimu kuibua hadithi za mafanikio za kujifunza za mfano zinazopatikana miongoni mwao ili kutatatua changamoto za ujifunzaji na ufundishaji ili kuinua ubora wa elimu nchini
Mafunzo hayo yaliendeshwa katika taasisi ya Ahlulbayt Islamic Centre yakihusisha Watendaji Kata, Waratibu Elimu Kata, Walimu Wakuu, na Walimu Wataaluma wa Shule za Msingi zilizopo Kata za Majengo, Kipampa, Businde na Rusimbi
Katika mafunzo hayo Watendaji kata walijadiliana na Walimu namna bora ya Ukuzaji elimu na ufaulu kwa kushirikisha Wazazi na Wadau wengine wa elimu katika maeneo yao
Aidha katika mafunzo hayo walijifunza namna kuibua hadithi za mafanikio za kujifunza kwa mfano kwa lengo la kuboresha ufundishaji na ujifunzaji
Mkufunzi na Mkuza mitaala kutoka taasisi ya elimu Tanzania Ndugu. Hwago Hassan Hwago alisema kutumia hadithi za mafanikio katika kufundisha na kujifunza zitamfanya mwanafunzi kuwa mbunifu ambapo atakuwa na uwezo wa kuibua tatizo, Ufumbuzi wa tatizo na kupata matokeo yaliyo bora
Mafunzo haya ya mradi wa Shule bora yanaendelea katika Halmashauri za Mikoa ya Kigoma, Singida, Katavi na Pwani kwa lengo la kukuza viwango vya elimu katika Mikoa hiyo yakiandaliwa na Mradi wa Shule unaofadhiliwa na mfuko wa Uk aids chini ya Usimamizi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
05/12/2022
Walimu na wasimamizi wa elimu Kata ya Mwanga Kusini na Kata ya Mwanga Kaskazini leo Desemba 05, 2022 wamehitimisha mafunzo kwa Walimu waliopo kazini (MEWAKA) baada ya Mafunzo hayo kuanza Jana Desemba 04, 2022
Mafunzo hayo yamehitimishwa katika Shule ya Msingi Muungano yalipokuwa yakifanyikia na yakiandaliwa na Mradi wa Shule unaofadhiliwa na mfuko wa Uk aids chini ya Usimamizi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Mikoa inayotekeleza mradi wa Shule bora ni pamoja na Mkoa wa Kigoma, Katavi, Dodoma, Mara, Pwani, Rukwa, Simiyu, Singida na Mkoa wa Tanga
04/12/2022
MAFUNZO YA SHULE BORA KWA WASIMAMIZI WA ELIMU NA WALIMU KAZINI KIGOMA/UJIJI
Posted On: December 4th, 2022
Na Mwandishi Wetu
Walimu na wasimamizi wa elimu ngazi ya kata wametakiwa kuibua hadithi za mfanikio za kujifunza kwa mfano kwa lengo la kuboresha ufundishaji na ujifunzaji kwa Wanafunzi katika mafunzo ya Siku mbili (02) yaliyoanza Leo Desemba 04, 2022 katika Shule ya Msingi Muungano
Ameyasema hayo Mkuza mitaala kutoka Taasisi ya Elimu Tanzania Ndugu. Hwago Hassan Hwago alipokuwa akitoa mafunzo kwa Walimu waliopo kazini (MEWAKA) yakihusisha Wasimamizi wa elimu ngazi ya kata na Walimu wa Shule za Msingi zilizopo Kata ya Mwanga Kusini na Kata ya Mwanga Kaskazini
Amesema hadithi za mafanikio ya kujifunza kwa mfano zinasaidia kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji, kutia moyo katika utendaji kazi, kuamsha ari ya kutenda kazi, na kukuza ushirikiano miongoni mwa wadau wa elimu
Amesema hadithi za mafanikio za kujifunza kwa mfano zinapatikana miongoni mwa Walimu, Jamii, Taasisi za Elimu, Viongozi wa dini, Wanasiasa na Wadau wote wa elimu
Mafunzo hayo yameandaliwa na Mradi wa Shule unaofadhiliwa na mfuko wa Uk aids chini ya Usimamizi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Miradi wa Shule bora unatekelezwa katika Mikoa tisa (9) Nchini Tanzania ukihusisha Halmashauri sitini na saba (67) na Shule elfu tano mia saba hamsini na saba ( 5, 757) na Unatarajia kuwanufaisha Wanafunzi zaidi ya Milioni tatu na laki nane ( 3, 800,000) na Walimu zaidi ya elfu hamsini na nne ( 54, 000)
Mikoa inayotekeleza mradi wa Shule bora ni pamoja na Mkoa wa Kigoma, Katavi, Dodoma, Mara, Pwani, Rukwa, Simiyu, Singida na Mkoa wa Tanga
03/12/2022
WIKI YA MAADHIMISHO MIAKA 61 YA UHURU WA TANZANIA BARA YAMEENDELEA KWA UPANDAJI MICHIKICHI KIGOMA/UJIJI
Posted On: December 3rd, 2022
Na Mwandishi Wetu
Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Leo Desemba 3, 2022 wameendelea na maazimisho ya wiki ya Sherehe ya Miaka sitini na Moja (61) tangu Tanzania bara awali ikiitwa Tanganyika ilipojipatia Uhuru wake Desemba 9, 1961
Maadhimisho hayo yameendelea kwa Wananchi, Viongozi na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kasimbu iliyopo katika Manispaa hiyo kushiriki zoezi la upandaji wa zao la Mchikichi
Akizungumza katika tukio hilo Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Idrisa Naumanga amewataka Wakazi wa Manispaa hiyo kuendelea na zoezi la upandaji wa miche ya kisasa ya zao hilo kutokana na uzalishaji wa mafuta ya Mawese kuwa mengi pamoja na malighafi zingine
Ameendelea kuwataka Wananchi kuendelea kuitunza na kuithamini miche hiyo iliyopandwa katika Shule ya Sekondari ikiwa ni alama ya kusherehekea miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania bara awali ikiitwa Tanganyika
Kaimu Mkurugenzi huyo ameiagiza idara ya Misitu na Mazingira kupandwa kwa miti mingine ya Matunda na kivuli katika Shule hiyo
Wakizungumza katika tukio hilo baadhi ya Wanafunzi wa Shule hiyo Ndugu. Ismail Samweli na Mashuma Swalehe wameipongeza Serikali kwa maadhimisho ya wiki ya Uhuru ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania bara huku wakisema mazao waliyopanda itakuwa ukumbusho huku wakiahidi kuilinda na kuitunza
Katika Shule hiyo zaidi ya Miche hamsini (50) ya Miche ya Kisasa ya zao la michikichi imepandwa na Wananchi, Walimu, Wanafunzi na Viongozi mbalimbali wa Kata na Mitaa walihudhuria maadhimisho hayo
Tanzania bara awali ikiitwa Tanganyika kwa sasa inafahamika kwa jina la Tanzania kutokana na Muungano wake na Zanzibar mwaka 1964 na Kauli mbiu ya Mwaka huu ni " Miaka 61 ya Uhuru, Amani na Umoja ni nguzo ya Maendeleo yetu ".
02/12/2022
Picha Mbalimbali za Wananchi na Wafanyabiashara wa Soko la Buzebazeba walipojitokeza Leo Desemba 02, 2022 katika ufanyaji Usafi katika Soko la Buzebazeba katika wiki ya maadhimisho ya Sherehe ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania bara
katika kuadhimisha maadhimisho hayo Kauli mbiu ya Mwaka huu ni " Miaka 61 ya Uhuru, Amani na Umoja ni nguzo ya Maendeleo yetu ".
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Contact the business
Website
Address
Kigoma
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 17:00 |
| Tuesday | 09:00 - 17:00 |
| Wednesday | 09:00 - 17:00 |
| Thursday | 09:00 - 17:00 |
| Friday | 09:00 - 17:00 |
