06/02/2026
UJENZI WA DARAJA LA MTO POLOLETI UMEKAMILIKA
Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Ngorongoro wamekamilisha ujenzi wa Daraja la Mto Pololeti lililopo katika Kata ya Oloipiri. Daraja hilo lina urefu wa mita 22 na limegharimu jumla ya shilingi 314,737,557.62, likiwa linaunganisha Kata ya Oloipiri na Soitsambu.
Ujenzi wa daraja hilo ulianza tarehe 6 Juni 2024 na kukamilika leo tarehe 6 Februari 2026. Kukamilika kwa daraja hili kunalenga kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi, hususan katika kipindi hiki cha msimu wa mvua, kwa kuhakikisha usalama na upatikanaji wa huduma kwa wakati.
TARURA inaendelea kutekeleza miradi ya miundombinu kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Wilaya ya Ngorongoro.

05/02/2026
29/01/2026
29/01/2026
28/01/2026