NYOTA YA Faraja

NYOTA YA Faraja

Share

Tunashughulika na mambo ya kijamii k**a Mahabusu, Wafungwa, Yatima, Wajane, Wazee na jamii kwa ujumla

10/02/2025

TAASISI YA NYOTA YA FARAJA KWA KUSHIRIKIANA NA TAASISI YA DARUL ISTIQAMA FOR ISLAMIC DEVELOPMENT

TUMEANZA KUPOKEA VIFAA MBALIMBALI KWA AJILI YA FUTARI KWA MAGEREZA YA UKONGA NA SEGEREA KWA AJILI YA FUTARI NA DAKU

UKONGA
WALIOTIA NIA NI - 620
- Kwa Siku watakula Mchele Kg. 155.
- Kwa Mwezi Watakula Mchele Kg. 4,650.
- Maharage Kg. 300
- Sembe Mifuko 10
- Tende Box 10
- Sukari Mifuko 5
- Tambi Box 5
- Mafuta ya Kula Dumu 3
- Viazi Mbatata Loba 2
- Kanzu Balo 2

SEGEREA
WALIOTIA NIA NI - 600
- Kwa Siku Watakula Mchele Kg. 150
- Kwa Mwezi Watakula Mchele Kg. 4,500
- Maharage Kg. 300
- Sembe Mifuko 10
- Tende Box 10
- Sukari Mifuko 5
- Tambi Box 5
- Ngano Mifuko 5
- Mafuta ya Kula Dumu 3

MAHITAJI MENGINE MUHIMU:
- MISAHAFU YA MATINI - 500
- JUZUU AMMA - 1,000
- MIKEKA YA KUSWALIA - 100
FIKISHA DUKANI KWA AL-HAJJ SAIMU GWAO MKABALA NA MSIKITI WA MTORO MKABIDHI USTADH. MUHIDINI

MICHANGO YOTE IPITIE: TANZANIA COMMERCIAL BANK AKAUNT NAMBA - 341204000409 AU LIPA NAMBA 7425770 JINA: DARUL ISTIQAMA FOR ISLAMIC DEVELOPMENT

AU WASILIANA NASI KWA NAMBA
0752249858
0785949076
(Hussein Mchomolo)
0715580807
(Kudura Sama)

FIKISHA SADAKA YAKO MASJID HAQQA BUGURUNI ROZANA MUULIZIE IMAMU HAMISI

NYOTA YA FARAJA
_Mwangaza kwa waliokata tamaa_
https://www.instagram.com/p/DF5BPbPIkCN/?igsh=MWd2YmdiYnhtMWwzOQ==

04/08/2022

Assalam alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh

Habarini la Majukumu

Kampeni yetu ya MSAHAFU WANGU bado inaendelea tusikose fadhila hizi, NUNUA MSAHAFU wako Fikisha Dukani kwa USTADH SAIMU GWAO Kariakoo Mkabala na Msikiti wa Mtoro

Wabillahi Tawfiq

30/11/2021

Assalam Alaykum Waramatullah wabarakatuh

NYOTA YA FARAJA

OMBI LA JUZUU AMMA NDOGO 300 NA MISAHAFU YA TAFSIRI YA KISWAHILI 10

Thamani ya Juzuu 1 @ ndogo ni 300 × 300 = 90,000/= na thamani ya Msahafu mmoja @ 10,000 × 10 = 100,000/=

Tunaomba tuendelee Kuchangia kwa ajili ya Vijana wetu, faida ya Kusomesha tena Qur'an fadhila zake sote tunazifahamu, tuwekeze kwa ajili ya Makaburi yetu na akhera yetu (Swadaqatul Jaalia)💰

Fikisha moja kwa moja Dukani kwa Ustadh. Saimu Gwao Mkabala na Msikiti wa Mtoto Kariakoo Mkabidhi Mwihidini

Au tupigie tutafwata ulipo Inshaa'allah, kwa namba zifuatazo:

0752249858, au 0776758241.

Au anayetaka kuchangia moja kwa moja, basi tuma Mchango wako kupitia
M - PESA 0752249858
: "Hussein Mchomolo"

Wabillahi Tawfiq

NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

24/11/2021

Assalam Alaykum Waramatullah wabarakatuh

TAARIFA YA ZIARA ZETU GEREZANI

Kwa ajili ya kuendelea kuutumikia Ummah hasa ndugu zetu walioko Mahabusu, Viongozi wa NYOTA YA FARAJA tumefanya Ziara katika Magereza ya Singida Mjini na Dodoma

Changamoto ni nyingi sana, kiasi tunalazimika wakati wote kuwaomba Waislamu waendelee Kutuunga Mkono kwa kujitolea kile walichojaaliwa ili walau kwa uchache tupunguze kwani hali iliyopo ni Mtihani


Bado kuna hitajio Kubwa la vitu Mbalimbali kwa ajili ya Mahabusu na Wafungwa, k**a vile
NGUO ZA KIUME NA ZA K**E, SABUNI ZA KUFULIA NA ZA KUOGEA, MISWAKI, DAWA ZA MENO

YA
Kuna mahitaji ya dharura yanatakiwa yawafikie ndugu zetu walioko Gereza la Singida, mahitaji hayo yako Dar, hivyo tunaomba Tupate fedha Tsh. 56,000/= kwa ajili ya Nauli ya Mtu mmoja ya kwenda tu, na nauli ya Mzigo

Vitu hivi vinatakiwa kesho kwa Tawfiq yake ALLAH vifike Singida Inshaa'allah, hivyo TUNAKUOMBA EWE NDUGU KATIKA IMANI kutuwezesha kiasi hicho cha Tsh. 56,000/=


Bado tunapokea vifaa mbalimbali kwa ajili ya ndugu zetu waliko Magerezani, vifaa hivyo ni:
NGUO ZA K**E NA KIUME (Kanzu/Hijabu) MADILA, VIATU, SABUNI, NK.

Kwa mawasiliano:
0752249858
0715580807

Wabillahi Tawfiq

NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

Photos from NYOTA YA Faraja's post 14/11/2021

Assalam alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh

MAOMBI YA KUPATIWA (Laptop)

Bado hatujapata!!
Ndugu zangu Waislamu tunaomba kwa yeyote Allah aliyemjaalia Uwezo na wasaa wa Kuifanya Kheri hii Muhimu kwa ajili ya wepesi wa Harakati zetu basi akimbilie kheri hii.

Tunashida sana ya ya aina yoyote, si lazima iwe MPYA hapana, tunataka hata Mtumba ila iwe mzima tu, itakuwa umetusaidia sana kwa Majukumu yetu

Allah anatunasihi:
"Na toeni katika tulivyo kupeni kabla hayajafikia mmoja wenu Mauti, tena hapo akasema: Mola wangu mlezi! Huniakhirishi muda kidogo nipate kutoa Sadaka, na niwe katika Watu wema?" (Q. 63:10)

Kwanini Ndugu yangu ufike wakati wa kujilaumu na Kujuta? Wakati ni sasa ukiwa Hai wekeza kwa ajili ya Nafsi yako na Akhera yako.

KWA YEYOTE ATAKAYEJAAIWA NA KHERI HII TUWASILIANE KWA NAMBA:

+255752249858

Wabillahi Tawfiq


NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

Photos from NYOTA YA Faraja's post 06/11/2021

BAADA YA KUTOKA MATOKEO YA DARASA LA SABA, WAZAZI AMBAO WATOTO WAO WAMEFAULU WAMEANZA KUHAMA MIJI KWA KUHOFIA KUSHIKWA ENDAPO WATOTO HAWATOENDA SHULE!!

NYOTA YA FARAJA
Tunaendelea Kukuomba wewe ambaye Mwenyezi Mungu amekujaalia nafasi basi tuwasaidie watoto Masikini na Mayatima

Hadi sasa tuna idadi ya Watoto 129 ambao Wazazi wao wamesema Bayana kuwa: "Wanahama Mjini na kwenda Mashambani kwani hawana uwezo wa Kuwasomesha watoto wao."

"Huyu mtoto amenileta Majanga, nilimwambia akifaulu atanifungisha, sina uwezo wa Kumsomesha, leo Majibu yametoka AMEFAULU!! Huyu mtoto!!" Alisikika Mzazi mmoja akimlaumu mtoto wake kwa nini amefaulu kwenda Sekondari.

Mwenye Jukumu la Kuwasaidia MAYATIMA na WASIO JIWEZA ni langu mimi na Wewe, tushirikiane ili watoto hawa January waweze kwenda Shule

Tunapokea Misaada kwa aina tatu

.
- TUNAPOKEA VIFAA K**A JOLA ZA VITAMBAA VIZITO KWA AJILI YA KUSHONA SKETI NA SURUALI, NA JOLA ZA VITAMBAA VYEUPE KWA AJILI YA KUSHONA MASHATI NA MAJUBA (SHUNGI) NA NUSU KANZU

- COUNTER BOOK, Q. II & III, MIKEBE, BIC, RULLA, PENSEL NK. GODORO 2½ × 6, TRANKA, SOKSI NYEUPE NA NYEUSI,


KWA YEYOTE MWENYE NIA YA KUMSIMAMIA MTOTO YATIMA KWA KUMSOMESHA (Kusimamia gharama zake zote hadi ana maliza kidato cha nne) IWE MMOJA AU WAWILI NA ZAIDI, , TAARIFA ZOTE ZA MTOTO ATAKUWA ANAPATIWA KILA HATUA.


- TUNAPOKEA PESA TASILIMU KWA LENGO LA KUFANIKISHA KUPATIKANA KWA GHARAMA ZA WATOTO HAWA MASIKINI.

SANA SANA KILA ALIYEJAALIWA CHOCHOTE BASI TUWASILIANE ILI TUWAWEZESHE HAWA WATOTO WATIMIZE NDOTO ZAO

KWA MICHANGO NA MAWASILIANO TUPIGIE:

0752249858 - M-PESA

Wabillahi Tawfiq

NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

13/10/2021

SAIDIA WASIO JIWEZA ILI WAENDE SEKONDARI KIDATO CHA KWANZA.

Siku chache zijazo, tutaanza pilikapilika za Maandalizi ya Watoto wetu kujiunga kidato cha kwanza, Imekuwa ni Kawaida kwa wale ambao hali zao za maisha ni duni kuhangaika huku na kule kutafuta misaada ya watoto wao waweze kwenda shule

NYOTA YA FARAJA kwa kulitambua hilo, tumeanza kukusanya vifaa mapema kwa ajili ya kuwasaida watoto Yatima na wale wasio na uwezo, vifaa vya shule ili na wao waripoti shule kwa wakati k**a wenzao.

: MAJOLA YA VITAMBAA VIZITO VYA RANGI TOFAUTI, NYEUSI, BLUE, DARK BLUE, KIJANI, NYEKUNDU, KIJIVU, RANGI YA UGOLO, DAMU YA MZEE NK

Pia : MADAFTARI, MIKEBE, KALAMU, BIKI, BEGI, VIATU, COUNTER BOOK Q. II pamoja na vifaa vingine muhimu pia pesa Taslimu.

Kwa yeyote atakayejaaliwa kuwa na nafasi ya kuchangia chochote basi wasiliana nasi kwa namba: 0752249858. Whatsapp na Kawaida

01/10/2021

Habari za Ijumaa

Tuendelee kushirikiana kusaidia jamii

Sisi tupo kwa ajili yako

Karibu sana

28/09/2021

Naam Wadau wetu habari za majukumu

Sisi tuko salama tunaendelea na jukumu la kuusaidia Ummah, karibu tushirikiane

12/08/2021

WEMA (SADAKA) UNALIPA, HAUPOTEI

SOMA KISA HIKI HALAFU CHUKUA HATUA.

Bilionea MNigeria Femi Otedola alipoulizwa kwenye interview, ya Simu na Mtangazaji wa Radio, "Sir ni kitu gani unachokumbuka kilichokufanya uwe na furaha maishani?"

Femi alijibu:
"Nimepitia hatua nne za furaha katika maisha yangu na mwishowe nilielewa maana ya furaha ya kweli."

Hatua ya Kwanza ilikuwa ni kutafuta Mali na kulimbikiza. Lakini katika hatua hii sikupata furaha niliyoihitaji.

Nikaingia hatua ya pili ya kujinunulia vitu vya thamani. Lakini niligundua kuwa vitu vyote hivi vinakupa furaha ya muda tu ambayo haidumu.

Nikaingia hatua ya tatu ya kufanya miradi mikubwa. Ni katika hatua hii nilikuwa ninasambaza 95% ya Diesel Nigeria yote na Africa Kwa ujumla. Pia nilikuwa mmiliki mkubwa wa Vessel Africa na Asia. Lakini pia hapa sikupata furaha niliyokuwa nimeifikiria.

Hatua ya nne ilikuwa ni kipindi ambacho Rafiki aliniomba kununua Wheelchairs Kwa ajili ya watoto walemavu. Walikuwa k**a watoto 200 hivi.

Baada ya kuombwa na rafiki yangu nilinunua Wheelchairs 200 mara moja.

Lakini pia aliniomba niambatane naye ili nikawakabidhi watoto zile wheelchairs. Nilijiandaa nikaambatana naye.

Nikawagawia zile wheel chairs Kwa mikono yangu mwenyewe. Niliona furaha ikitawala kwenye nyuso za hawa watoto. Nikawaona wamekaa kwenye wheelchairs, wakizunguka na kufurahia.

Ilikuwa ni k**a wako Picnic wakisherehekea ushindi wa bahati nasibu.

NiIihisi furaha ya kweli ndani yangu. Nilipotaka kuondoka mtoto mmoja alinishika miguu yangu. Nilijaribu kujinasua taratibu lakini alinikazia macho akinitazama usoni.

Niliinama chini nikamuuliza, kuna kitu kingine unahitaji?

Jibu alilolitoa mtoto huyu sio tu kwamba lilinipa furaha bali pia lilinifanya nibadili kabisa mtazamo wangu juu ya maisha. Mtoto huyu alisema:
"Ninakuangalia ili niikumbuke Sura yako, siku nikikukuta mbinguni niweze kukutambua na kukushukuru tena."

Je Wewe mwenzangu, utakumbukwa Kwa lipi utakapoondoka kwenye hiyo Kampuni, Ofisi, Biashara, Kazini au mahali unapoishi?
Je kuna Mtu atatamani kuuona uso wako tena siku za usoni?.

27/07/2021

Assalam alaykum warahmatullah wabarakatuh

NYOTA YA FARAJA

HARAMBEE YA SIKU 10. YA UKUSANYAJI WA NGUO ZA K**E NA ZA KIUME, TAULO ZA K**E, JUZUU KUBWA NA NDOGO, SABUNI ZA KUOGEA, SABUNI ZA UNGA, SABUNI ZA USAFI, DAWA ZA MENO, MISWAKI NA DAWA ZA U.T.I

Leo tarehe 04/08/2021 ni Siku ya Tisa (9) ya Harambee. SHIME tuendee Kuchangia

Tumeanza kupokea vitu tajwa hapo juu kwa ajili ya ndugu zetu katika Imani WAFUNGWA na MAHABUSU


Tunapokea Kanzu, Misuli, Mashati, Suruali, Fulana (zisiwe za picha na Maandishi)

**E
Tunapokea Hijabu, Majuba, Madila, Mitandio, Taulo za K**e (Hitajio kubwa sana)

VITU VINGINE ni pamoja na MISAHAFU ya Matini na Tafsiri, JUZUU kubwa na ndogo, Sabuni za Kuogea, Sabuni za Usafi, Dawa za Meno, Miswaki.

MISAHAFU na JUZUU zifikishwe Kariakoo Dukani kwa Ustadh Saimu Gwao Muulize Muhidini

NGUO na Vitu vingine vifikishwe MASJID HAQQA Buguruni ROZANA Mkabidhi IMAMU HAMISI.

FAHAMU KUWA: "Nguo unayofikiria kuifanya Dekio, basi kwa wenzio ni Mpya"

AU TUPIGIE TUTAFWATA POPOTE ULIPO MZIGO KWA DAR ES SALAAM

KWA MWENYE NIA YA KUTOA CHOCHOTE ALICHO JAALIWA BASI TUMA KATIKA MOJA YA NAMBA HIZI HAPA CHINI

M - pesa - 0752249858 - Sheikh Mchomolo
Tigo Pesa - 0715580807 - Kudura Sama.

Wabillahi Tawfiq

NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

02/07/2021

Assalam alaykum warahmatullah wabarakatuh

NYOTA YA FARAJA

MCHANGO! MCHANGO!
✍🏻 VIFAA VYA UJENZI WA MSIKITI.

Mtume (s.a.w) amesema:
Mwenye Kujenga Msikiti kwa sababu ya Kumpenda Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu atamjengea JENGO Kubwa Peponi" (Muslim)

TUNAWASHUKURU MNAO CHANGIA ILI KUPATA VIFAA TUENDELEE KUCHANGIA TUKAMILISHE

🌸MAHITAJI KWA SASA NI K**A IFUATAVYO:

1. BORITI
▶️ Boriti - 2/4. - 50 @ 4,800 Sawa 480,000/=
▶️ Boriti - 2/2. - 100 @ 4,000 Sawa Tsh. 400,000/=

2. BATI
▶️ Bati 35 (G' 30) @ 19,000 Sawa Tsh. 760,000/=

3. MIKEKA
▶️ Mikeka ya Kuswalia 96 @ 15,000. Sawa Tsh. 1,440,000/=

✍🏻 TUPIGIE/TUMA MCHANGO WAKO:

Mpesa 0752249858
Airtel Money 0785949076

Wabillahi Tawfiq

NYOTA YA FARAJA
Mwangaza kwa waliokata tamaa

Want your business to be the top-listed Government Service in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 16:00
Saturday 09:00 - 15:00
Sunday 09:00 - 13:00