25/01/2019
Tanzia: Nguli wa Tasnia ya Filamu na Michezo ya Kuigiza nchini Bi. Salome Nonge maarufu kwa jina la Mama Abduli amefariki dunia leo Tarehe 25 Januari, 2019 akiwa nyumbani kwake Mburahati jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa ini.
11/01/2019
Tunapongeza jitihada chanya za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anazozionesha katika kukuza na kuendeleza uchumi wa Taifa letu kwa kufanikisha ununuzi wa ndege hii yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 160. Hongera Mhe. Rais kwa kuudhihirishia Ulimwengu Uwezo wa Tanzania ambapo kwa pamoja tunasema "Tanzania Roho Ya Afrika, Anga Linashangilia"
Kununuliwa kwa Ndege hii kutafungua fursa nyingi za kiuchumi nchini kupitia Sekta mbalimbali k**a Usafirishaji na Uchukuzi, Utalii, Biashara, Filamu na zaidi kuimarisha azma ya kufikia uchumi wa Viwanda.
Aidha kupitia uwekezaji huu utarahisisha Mawasiliano na Uchukuzi kwa kuruhusu Watendaji katika Sekta ya Filamu na Michezo ya Kuigiza kwa kutembelea Tanzania na kufanya kazi kwa wakati kutoka eneo moja kwenda lingine kutokana na uhakika wa usafiri bora wa anga.
02/10/2017
Bodi ya Filamu Tanzania imetunukiwa cheti cha udhamini kwenye kilele cha 36 cha Tamasha la Kimataifa la Utamaduni na Sanaa Bagamoyo. Mgeni rasmi kwenye kilele hicho Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson alimkabidhi Katibu Mtendaji wa kwa niaba ya TaSUBA
20/07/2017
Mwanafamilia mpya kwenye ukurasa wetu karibun sana. Kupitia ukurasa huu utapata taairfa mbalimbali zinazohusu Bodi ya Filamu Tanzania na sekta ya filamu nchini Tanzania.
Bodi ya Filamu Tanzania
Huu ni ukarasa rasmi wa Bodi ya Filamu Tanzania. Kupitia ukurasa huu unaweza kupata habari na picha za matukio mbalimbali ya Bodi ya Filamu Tanzania, pia kupitia ukurasa huu unaweza kuwasilisha maoni, maswali, hoja na mapendekezo yako.
28/06/2017
Wana familia wapya kwenye familia yetu kubwa ya Bodi ya Filamu Tanzania tunawakaribisha. Mjisikie mko nyumbani. Tuendelee kupashana habari na kufungua fursa zinazopatikana kwenye tasnia ya filamu nchini Tanzania.
Bodi ya Filamu Tanzania
Huu ni ukarasa rasmi wa Bodi ya Filamu Tanzania. Kupitia ukurasa huu unaweza kupata habari na picha za matukio mbalimbali ya Bodi ya Filamu Tanzania, pia kupitia ukurasa huu unaweza kuwasilisha maoni, maswali, hoja na mapendekezo yako.
09/06/2017
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Joyce Fissoo amemtembelea na kufanya mazungumzo na Naibu Balozi wa China ofisi kwake leo. Kwenye mazungumzo hayo Ubalozi wa China umeonyesha nia ya kushirikiana na Bodi ya Filamu Tanzania kuongeza masoko ya filamu za Tanzania nchini China, kushirikiana kutengeneza filamu, kubadilishana uzoefu na kutoa nafasi za mafunzo kwa wadau mbalimbali wa sekta ya filamu nchini
01/06/2017
VIJANA WAPENDA FILAMU JITOKEZENI KWA WINGI