Ujumbe wa leo: Ugonjwa wa Kisukari
Tunasisitizwa sana kufanya mazoezi kwa takriban nusu saa kwa siku na ambayo mtu anatoa jasho na moyo kumwenda mbio. Hiyo ni kwa ajili ya kusaidia misuli ya miguu, tumbo, kifua, mgongo na mikono kutumia kiasi cha sukari kinachozalishwa mwilini. Kadhalika, wataalamu wanasisitiza sana kula vyakula visivyokobolewa, ikiwamo kula dona badala ya sembe, ulezi, mtama na matunda. Watu wapunguze na ikiwezekana kuacha kunywa vimiminika vyenye sukari, ikiwamo juice, soda, pombe na vinginevyo. Na hiyo ni kwasababu vinywaji hivyo havikai tumboni na badala yake huenda moja kwa moja kwenye utumbo mwembamba na kulazimisha kongosho linalozalisha kemikali ya insulin kufanya kazi kwa kiwango cha juu kuliko ilivyo kawaida. Vyakula visivyokobolewa vina faida sana kwani vinachukua muda wa kutosha kutoka kwenye tumbo na kwenda kwenye utumbo mwembamba hatimaye kuvunjwavunjwa kwa ajili ya kutumika mwilini.
Kadhalika makapi yatokanayo na hivyo vyakula hutuzuia kupata kansa ya utumbo. La ajabu wametoa takwimu za kutisha kwani ulaya kwasababu wanakula vyakula vilivyokobolewa wanapata kansa ya utumbo kuliko nchi au bara la afrika, na kansa hiyo ni ya nne kwa kusababisha vifo barani ulaya na amerika.
Tafadhalini, tujihadhari kwa afya zetu; mazoezi ni muhimu, vyakula viwe na uasilia wake, mtu aliye na mwenza wake afanye tendo la ndoa kwa kadiri inavyowezekana kwani ni sehemu ya mazoezi, tubadili mifumo ya maisha yetu na kukaa tu bila kujishughulisha mili yetu.
Tunawatakia wiki njema na afya njema.
Muhimbili National Hospital
MNH is National Referral Hospital and University Teaching Hospital
Today's Message: Children Malnutrition
To avoid malnutrition for your new born baby consider the following tips; Exclusive breastfeeding for the first 6 months, timely complementation that means feeding the baby with food that contains other nutrients for the first 6 months of age while continuing with breastfeeding for 2 years or more,you are encouraged to visit the hospital often for improvement of services for growth monitoring and vaccinations as well as to prevent/early treatment of illnesses such as diarrhoea, pneumonia, etc and last but not least to the mother-Eat a healthy balanced diet.
Sincerely,
Moderator.
14/11/2014
8th March 2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
14/11/2014
Foreign Liason
14/11/2014
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Contact the business
Website
Address
Muhimbili
Dar Es Salaam
