Baraza la Masoko ya Mitaji - CMT Tanzania

Baraza la Masoko ya Mitaji - CMT Tanzania

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Baraza la Masoko ya Mitaji - CMT Tanzania, Government Organization, S. L. P 1384 Ghorofa ya Kwanza, Hazina Ndogo, Dar es Salaam (Posta-Mtaa wa Madaraka), Dar es Salaam.

The page is all about what is done by the Capital Market Tribunal (CMT) towards ensuring fair and timely adjudication of disputes and controversies within the capital markets.

30/05/2026

Mapinduzi ya Kidijitali: Mfumo Mpya wa Usimamizi wa Mashauri (CMS)

​Wakati wa Mafunzo ya Mawakili wa Serikali 2026 yaliyofanyika na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, ilionyeshwa video inayotambulisha Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT Case Management System).

Video hiyo ilionyesha muonekano, sifa na faida za mfumo huo wa kidijitali.

​Lengo ni kurahisisha upatikanaji wa haki kwa njia ya kiteknolojia na kuongeza ufanisi katika usimamizi na utatuzi wa mashauri ya masoko ya mitaji, dhamana na bidhaa nchini.

27/05/2026
25/05/2026

Utatuzi wa Migogoro na Muundo wa Masoko ya Mitaji, Dhamana na Bidhaa

​Mnamo tarehe 19 Mei 2026, Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Mhe. Dkt. Martin Kolikoli, aliwasilisha mada katika Mafunzo ya Mawakili wa Serikali yaliyofanyika na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

​Wasilisho lake lilihusisha mfumo wa utatuzi wa migogoro katika soko la bidhaa, majukumu yanayotekelezwa na CMSA, TMX na DSE, pamoja na wadau na bidhaa zilizopo katika sekta ya masoko ya mitaji, dhamana na bidhaa.

​Hii ni katika kuwajengea uwezo Mawakili wa Serikali kupitia maarifa maalumu ili kuhakikisha utatuzi wa migogoro ya kifedha na kibiashara unafanyika kwa ufanisi.

22/05/2026

Kuimarisha Utatuzi wa Migogoro katika Sekta ya Fedha

Mnamo tarehe 19 Mei 2026, Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Mhe. Dkt. Martin Kolikoli, aliwasilisha mada katika Mafunzo ya Mawakili wa Serikali yaliyofanyika na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

Wasilisho lake lilihusisha muundo na majukumu ya Wajumbe wa Baraza, mamlaka ya Baraza juu ya masoko ya mitaji, dhamana na bidhaa katika Tanzania Bara na Zanzibar, pamoja na miongozo ya uwasilishaji wa mashauri na muda wa kisheria uliowekwa.

Hii ni katika kuwajengea uwezo Mawakili wa Serikali kupitia maarifa maalumu ili kuhakikisha utatuzi wa migogoro ya kifedha na kibiashara unafanyika kwa ufanisi.


22/05/2026

Kuimarisha Utatuzi wa Migogoro katika Sekta ya Fedha

Mnamo tarehe 19 Mei 2026, Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Mhe. Dkt. Martin Kolikoli, aliwasilisha mada katika Mafunzo ya Mawakili wa Serikali yaliyofanyika na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

Wasilisho lake lilihusisha muundo na majukumu ya Wajumbe wa Baraza, mamlaka ya Baraza juu ya masoko ya mitaji, dhamana na bidhaa katika Tanzania Bara na Zanzibar, pamoja na miongozo ya uwasilishaji wa mashauri na muda wa kisheria uliowekwa.

Hii ni katika kuwajengea uwezo Mawakili wa Serikali kupitia maarifa maalumu ili kuhakikisha utatuzi wa migogoro ya kifedha na kibiashara unafanyika kwa ufanisi.

Photos from Baraza la Masoko ya Mitaji - CMT Tanzania's post 20/05/2026

Umahiri katika Utetezi wa Ki-Utendaji wa Kimahakama (Quasi-Judicial Advocacy)

Mnamo tarehe 19 Mei 2026, Mhe. Rose Ebrahim (Jaji Mfawidhi wa Makama Kuu ya Tanzania - Masjala Ndogo ya Morogoro) alikuwa mwasilisha mada mkuu katika Mafunzo ya Mawakili wa Serikali ya Mwaka 2026, akiwasilisha mada kuhusu utendaji, taratibu na usimamizi wa sheria kwenye majukwaa ya udhibiti.

Kikao hicho kilichojaa maarifa kiliongozwa vyema na Mhe. Salma Maghimbi (Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania - Masjala Ndogo ya Dar es Salaam), kikiwashirikisha wachambuzi (panelists) Bw. Deodatus Nyoni (Mkurugenzi Msaidizi wa Mashauri ya Ndani ya Nchi - OSG) na Mhe. Dkt. Martin Kolikoli (Msajili wa Baraza la Soko la Mitaji - CMT).

Baraza linatoa shukrani za dhati kwa Wakili Mkuu wa Serikali kwa kutoa jukwaa hili zuri la kubadilishana ujuzi na kuimarisha utetezi katika masuala ya udhibiti.

16/05/2026

Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri wa CMT

Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT) linakuletea Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri (CMS). Sasa unaweza kuanzisha mashauri, kuwasilisha majibu bila karatasi, kuomba kuongezewa muda na kufuatilia mwenendo wa shauri lako kwa uwazi wa wakati halisi (real-time) popote ulipo duniani.

Anza kutumia sasa: cms.cmt.go.tz/login

14/05/2026

CMT na Jumuiya ya Kimataifa

Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT) linaandaa kipindi mubashara la mtandaoni (webinar) kupitia https://meet.google.com/dey-kmae-fze Jumamosi hii, Mei 16, saa 1:00 usiku (19:00 EAT) kwa ajili ya Watanzania waishio nje ya nchi (diaspora) kote Ulaya, Mashariki ya Kati, Afrika na Asia.

Kipindi hichi maalum utahusisha muhtasari wa mamlaka ya Baraza (CMT) na utambulisho wa Mfumo wa Kidijitali wa Kusimamia Mashauri (CMS).

Tunawakaribisha kujumuika nasi katika kukuza na kuongeza ujumuishi kwenye sekta ya fedha.

10/05/2026

Mubashara kupitia Uhuru FM: Nafasi ya CMT katika Mustakabali wa Kifedha wa Tanzania

Mnamo tarehe 12 Mei 2026, Msajili wa Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Mhe. Dkt. Martin Kolikoli atakuwa mubashara kupitia Uhuru FM.

Mazungumzo hayo yatahusisha uanzishwaji, mamlaka ya Baraza, michakato ya rufaa, pamoja na mfumo wa usimamizi wa mashauri kwa njia ya mtandao.

Pia, Msajili atafafanua nafasi ya CMT katika kuisaidia Tanzania kufikia njia mbadala za upatikanaji wa mitaji na utekelezaji wa malengo yaliyowekwa chini ya Dira ya Taifa 2050.

Want your business to be the top-listed Government Service in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address


S. L. P 1384 Ghorofa Ya Kwanza, Hazina Ndogo, Dar Es Salaam (Posta-Mtaa Wa Madaraka)
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30