Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania

Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania

Share

Tume ya Utumishi wa Walimu ni Mamlaka ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari

TSC Yawaaga Wachezaji Wanaokwenda SHIMIWI Mwanza

Na Mwandishi wetu, Dodoma.
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl. Paulina Nkwama, tarehe 29 Agosti 2025, amewaaga rasmi wachezaji wa Tume watakaoshiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza.
Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Tume, Makao Makuu, Mwl. Nkwama aliwataka washiriki hao kuzingatia miiko na maadili ya Utumishi wa Umma katika kipindi chote cha michezo hiyo.
“Haijawahi kutokea na wala sitarajii kusikia kwa upande wetu kuwa mtumishi wa Tume anajihusisha na vitendo vinavyokiuka maadili ya utumishi wa umma. Hakikisheni mnazingatia malengo yaliyowapeleka huko,” alisema Katibu huyo.
Timu ya TSC yenye zaidi ya wachezaji 14 itashiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete, kurusha tufe, mbio za baiskeli, riadha, bao na draft.
Katika hatua nyingine, Katibu wa Tume alipokea kikombe na medali kutoka kwa washindi wa mashindano ya Mei Mosi mwaka huu. Miongoni mwa washindi hao ni Pulkeria Mwaimu, aliyenyakua kombe katika mchezo wa draft kwa upande wa wanawake, na Enid Geofrey, aliyeshika nafasi ya pili katika mchezo wa kurusha tufe.
Mwl. Nkwama aliwapongeza washindi hao akibainisha kuwa wameitangaza vyema Tume kupitia michezo, huku akihimiza watumishi wote wa Tume kupenda michezo na kufanya mazoezi mara kwa mara kwa ajili ya kujenga afya bora.
Awali, Mwenyekiti wa Michezo wa TSC, Mwl. Mectildis Kapinga, alieleza kuwa wanamichezo wengine wa Tume walioshiriki katika michezo ya Mei Mosi licha ya kutopata vikombe na medali walifanya vizuri kwa kuingia katika kumi bora kwenye michezo waliyoshiriki. 
Aidha, mchezaji Debora Chambo akitoa neno la shukrani alisema, “Tunaishukuru Menejimenti ya Tume kwa kuipa michezo kipaumbele. Wachezaji wote tuna ari kubwa ya mashindano haya, na matarajio yetu ni kufanya vizuri na kuiletea Tume ushindi.”
Mashindano ya SHIMIWI yanatarajiwa kutoa fursa ya kuonyesha vipaji vya michezo pamoja na kukuza afya na mshik**ano miongoni mwa watumishi wa umma. 29/08/2025

TSC Yawaaga Wachezaji Wanaokwenda SHIMIWI Mwanza Na Mwandishi wetu, Dodoma. Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Mwl. Paulina Nkwama, tarehe 29 Agosti 2025, amewaaga rasmi wachezaji wa Tume watakaoshiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza. Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Tume, Makao Makuu, Mwl. Nkwama aliwataka washiriki hao kuzingatia miiko na maadili ya Utumishi wa Umma katika kipindi chote cha michezo hiyo. “Haijawahi kutokea na wala sitarajii kusikia kwa upande wetu kuwa mtumishi wa Tume anajihusisha na vitendo vinavyokiuka maadili ya utumishi wa umma. Hakikisheni mnazingatia malengo yaliyowapeleka huko,” alisema Katibu huyo. Timu ya TSC yenye zaidi ya wachezaji 14 itashiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete, kurusha tufe, mbio za baiskeli, riadha, bao na draft. Katika hatua nyingine, Katibu wa Tume alipokea kikombe na medali kutoka kwa washindi wa mashindano ya Mei Mosi mwaka huu. Miongoni mwa washindi hao ni Pulkeria Mwaimu, aliyenyakua kombe katika mchezo wa draft kwa upande wa wanawake, na Enid Geofrey, aliyeshika nafasi ya pili katika mchezo wa kurusha tufe. Mwl. Nkwama aliwapongeza washindi hao akibainisha kuwa wameitangaza vyema Tume kupitia michezo, huku akihimiza watumishi wote wa Tume kupenda michezo na kufanya mazoezi mara kwa mara kwa ajili ya kujenga afya bora. Awali, Mwenyekiti wa Michezo wa TSC, Mwl. Mectildis Kapinga, alieleza kuwa wanamichezo wengine wa Tume walioshiriki katika michezo ya Mei Mosi licha ya kutopata vikombe na medali walifanya vizuri kwa kuingia katika kumi bora kwenye michezo waliyoshiriki. Aidha, mchezaji Debora Chambo akitoa neno la shukrani alisema, “Tunaishukuru Menejimenti ya Tume kwa kuipa michezo kipaumbele. Wachezaji wote tuna ari kubwa ya mashindano haya, na matarajio yetu ni kufanya vizuri na kuiletea Tume ushindi.” Mashindano ya SHIMIWI yanatarajiwa kutoa fursa ya kuonyesha vipaji vya michezo pamoja na kukuza afya na mshik**ano miongoni mwa watumishi wa umma.

TSC YAKUTANA NA UONGOZI WA CWT NGAZI YA TAIFA KUIMARISHA HUDUMA KWA WALIMU

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) tarehe 22 Agosti, 2025 imefanya kikao na Uongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ngazi ya Taifa jijini Dodoma, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma bora kwa walimu.

Kikao hicho kiliongozwa na Katibu wa Tume, Mwl. Paulina Nkwama, ambaye alisisitiza kuwa CWT, k**a chombo cha walimu nchini, ni mdau muhimu katika kuhakikisha walimu wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia miiko na maadili ya kazi hiyo.

“CWT ni mdau muhimu wa TSC. Lengo letu ni kuhakikisha walimu wanahudumiwa kwa ubora zaidi, wakiwa na uelewa wa kutosha juu ya wajibu wao kazini ili kuepusha ukiukaji wa taratibu za utumishi,” alisema Mwl. Nkwama.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Elimu na Mafunzo Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bi Stella Kiabo aliipongeza Tume kwa kushirikisha chama hicho katika masuala yanayohusu maendeleo ya walimu, alisisitiza kuwa mshik**ano huo utaboresha maslahi na ari ya walimu nchini.

“TSC na CWT tukishirikiana kwa karibu, walimu watanufaika zaidi kwa kupata huduma stahiki na haki zao za msingi. Ushirikiano huu pia utasaidia kutatua changamoto zinazowakabili walimu kwa haraka zaidi,” alisema Bi Kiabo.

Aidha, viongozi wa pande zote mbili walisema kuwa, ili kufanikisha malengo ya elimu nchini, ni muhimu kushirikiana kwa nguvu zote.

“Wote tunamlenga mwalimu, hivyo tunahitaji nguvu ya pamoja kuhakikisha mwalimu anatimiza wajibu wake na kupata haki zake,” walieleza.

CWT pia wamepongeza Tume kwa kuwa na sala ambayo hufanyika kabla ya kuanza kwa shughuli rasmi siku husika, ikichangia kuimarisha maadili, haki na uwajibikaji wa watumishi wa Tume katika kutekeleza majukumu yao. 

Kupitia kikao hiki, pande zote mbili zimeahidi kuendeleza mashauriano ya mara kwa mara ili kujenga mazingira rafiki ya utumishi, kuongeza ufanisi wa walimu kazini, na hatimaye kuinua ubora wa elimu nchini.@ikulu_mawasiliano @ortamisemi @chama_cha_walimu_tanzania1 #tanzania #teacher #walimu #elimu 26/08/2025

TSC YAKUTANA NA UONGOZI WA CWT NGAZI YA TAIFA KUIMARISHA HUDUMA KWA WALIMU Na Mwandishi Wetu, Dodoma Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) tarehe 22 Agosti, 2025 imefanya kikao na Uongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ngazi ya Taifa jijini Dodoma, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma bora kwa walimu. Kikao hicho kiliongozwa na Katibu wa Tume, Mwl. Paulina Nkwama, ambaye alisisitiza kuwa CWT, k**a chombo cha walimu nchini, ni mdau muhimu katika kuhakikisha walimu wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia miiko na maadili ya kazi hiyo. “CWT ni mdau muhimu wa TSC. Lengo letu ni kuhakikisha walimu wanahudumiwa kwa ubora zaidi, wakiwa na uelewa wa kutosha juu ya wajibu wao kazini ili kuepusha ukiukaji wa taratibu za utumishi,” alisema Mwl. Nkwama. Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Elimu na Mafunzo Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bi Stella Kiabo aliipongeza Tume kwa kushirikisha chama hicho katika masuala yanayohusu maendeleo ya walimu, alisisitiza kuwa mshik**ano huo utaboresha maslahi na ari ya walimu nchini. “TSC na CWT tukishirikiana kwa karibu, walimu watanufaika zaidi kwa kupata huduma stahiki na haki zao za msingi. Ushirikiano huu pia utasaidia kutatua changamoto zinazowakabili walimu kwa haraka zaidi,” alisema Bi Kiabo. Aidha, viongozi wa pande zote mbili walisema kuwa, ili kufanikisha malengo ya elimu nchini, ni muhimu kushirikiana kwa nguvu zote. “Wote tunamlenga mwalimu, hivyo tunahitaji nguvu ya pamoja kuhakikisha mwalimu anatimiza wajibu wake na kupata haki zake,” walieleza. CWT pia wamepongeza Tume kwa kuwa na sala ambayo hufanyika kabla ya kuanza kwa shughuli rasmi siku husika, ikichangia kuimarisha maadili, haki na uwajibikaji wa watumishi wa Tume katika kutekeleza majukumu yao. Kupitia kikao hiki, pande zote mbili zimeahidi kuendeleza mashauriano ya mara kwa mara ili kujenga mazingira rafiki ya utumishi, kuongeza ufanisi wa walimu kazini, na hatimaye kuinua ubora wa elimu nchini.@ikulu_mawasiliano @ortamisemi @chama_cha_walimu_tanzania1 #tanzania #teacher #walimu #elimu

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 13/02/2024

SERIKALI KUENDELEA KUONGEZA NGUVU KATIKA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KUKABILIANA NA UPUNGUFU WA WALIMUI

Serikali imesisitiza kuendelea kuweka nguvu kwenye matumizi ya teknolojia katika kutoa elimu shuleni ikiwa ni moja ya njia za kukabiliana na changamoto ya upungufu wa walimu nchini.

Hayo yamesemwa Februari 12, 2024 na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Dkt. Charles Msonde wakati alipotembelewa na ujumbe wa wataalamu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ya Serikali ya Mapindinduzi ya Zanzibar ambao wamefanya ziara Tume ya Utumishi wa Walimu kwa lengo la kujifunza namna Tume hiyo inavyotekeleza majukumu yake.

Dkt. Msonde alisema Serikali chini ya Utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan imefanya jitihada mbalimbali za kuboresha elimu ili kuhakikisha kila mwanafunzi anapata elimu k**a inavyohitajika.

“Kwa sasa tumeanza majaribio ya matumizi ya teknolojia ya ufundishaji inayowezesha Mwalimu kutoka kituo kimoja kufundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja wakiwa katika maeneo mbalimbali. Tumeanza majaribio haya katika Mikoa miwili ya Pwani na Dodoma na kwa kweli matokeo yake ni mazuri na wanafunzi wanafurahia,” alisema Dkt, Msonde.

Aliongeza kuwa, “kupitia teknolojia hiyo mwalimu anaona wanafunzi wake wote katika maeneo mbalimbali, anaweza kuuliza swali na mwanafunzi akanyoosha mkono na kujibu, yaani ni k**a vile mwalimu yupo hapo hapo.”

Naibu Katibu Mkuu huyo aliongeza kuwa mbali na mfumo huo kurahisisha utendaji kazi kwa walimu, ni moja ya njia za kukabiliana na upungufu wa walimu hususan wa masomo ya Sayansi na Hisabati.

Ameongeza kuwa katika kuendeleza jitihada hizo, Waziri wa Nchi OR – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) tayari ameagiza kutengwa kwa bajeti ili kuwezesha upatikanaji wa angalau darasa moja kwa kila Mkoa na kila Halmashauri katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Pamoja na hayo, Dkt. Msonde alieleza kuwa TSC imeendelea kusimamia masuala ya utumishi wa walimu kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kusimamia ajira, maadili na maendeleo ya walimu ambapo hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa ili kumaliza malalamiko ya walimu.
@mohamed_mchengerwa

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 13/02/2024

WATAALAM WA ELIMU KUTOKA ZANZIBAR WATEMBELEA TSC KUJIFUNZA NAMNA INAVYOFANYA KAZI

Wataalam kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Februari 12, 2024 wametembelea Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kwa lengo la kupata uzoefu wa namna TSC inavyotekeleza majukumu yake katika kuhudumia walimu.

Ujumbe huo ulipokelewa na Katibu wa TSC, Mwl. Paulina Nkwama na kisha kufanya kikao na Menejimenti ya TSC ambapo pamoja na mambo mengine Mwl. Nkwama aliwaeleza wataalam hao kuwa Tume hiyo imeanzishwa kwa Sheria Sura 448 kwa lengo la kusimamia walimu wa Shule za Msingi na Sekondari walio kwenye Utumishi wa Umma Tanzania Bara.

“Tume yetu inasimamia masuala ya Ajira, Maadili na Maendeleo ya Walimu. Tume hii inahusika na mwalimu tangu anapoingia kazini hadi anapostaafu kwa maana tunashughulika na ajira yake, tunamthibitisha kazini, tunampandisha cheo, tunambadilishia cheo pale anapojiendeleza kielimu na kutimiza vigezo, tunatoa kibali cha kustaafu lakini pia tunasimamia nidhamu na maadili yake,” alisema Katibu huyo.

Nkwama aliongeza kuwa kwa mujibu wa Sheria hiyo, TSC ina ofisi katika wilaya zote 139 za Tanzania Bara ambapo ofisi hizo ndizo zinazomhudumia mwalimu moja kwa moja jambo ambalo limesaidia kurahisisha mwalimu kupata huduma.

Aliongeza kuwa TSC kwa kushirikiana na Mamlaka zingine imesaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa njia mbalimbali ikiwemo kuanzisha Mfumo wa Teachers’ Service Commission Management Information System (TSCMIS) ambao unamfanya mwalimu kuwasilisha changamoto zake kwa kutumia simu yake ya mkononi bila kutoka kwenye kituo cha kazi.

Kwa upande wake, kiongozi wa ujumbe huo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Bi. Mtumwa Iddi Hamad alimshukuru Katibu wa TSC pamoja na Menejimenti ya Tume kwa kukubali kuwapokea na kuwapa uzoefu wa namna kazi zinavyofanyika katika chombo hicho cha kuhudumia walimu.

Alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakusudia kuanzisha chambo cha kusimamia walimu tofauti na sasa ambapo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ndiyo inayosimamia walimu moja kwa moja.

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 07/02/2024

Maafisa Rasilimali Watu kutoka Halmashauri zote 184 nchini wakishirikiana na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais - Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na TAMISEMI wakiendelea na kazi maalum ya kuhuisha taarifa na kupakia taarifa sahihi za Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari za Umma ili kukabiliana na changamoto ya malalamiko ya upandaji vyeo na kubadilisha kazi/ vyeo ili Serikali iweze kuchukua maamuzi na hatua stahiki ya kumaliza kabisa changamoto hiyo. Kazi hiyo inaendelea kwa siku 14 kuanzia Jumatano ya tarehe 31.01.2024 Jijini Dodoma.

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 07/02/2024

MCHENGERWA AZINDUA MFUMO WA UFUNDISHAJI MUBASHARA (SMART CLASSES)

SERIKALI imeanza majaribio ya mfumo wa ufundishaji mbashara ambao mwalimu mmoja anaweza kufundisha wanafunzi wa nchi nzima kwa wakati mmoja.

Mfumo huo ambao kwa sasa unafanyiwa majaribio kwa baadhi ya shule za mikoa miwili ya Pwani na Dodoma, unamwezesha mwalimu kutoka kituo kimoja kufundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja wakiwa mikoa tofauti.

Utaratibu huo unaleta tafsiri ya kwamba mbali na kurahisisha utendaji kazi, pia ni njia mojawapo ya kukabiliana na uhaba wa walimu, hasa wa masomo ya sayansi shuleni.

Wakati Serikali inaendelea na majaribio ya mfumo huo, wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Dodom wamesema mfumo huo utawasaidia kupata uelewa kwa wepesi na kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa.

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 28/01/2024

Hongera sana kwa walimu wote nchini.

28/01/2024

Kheri ya kuzaliwa Rais wetu mpendwa.

28/01/2024

Pongezi nyingi kwa walimu nchini.

Photos from Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania's post 05/01/2024

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonazi amepokea msaada wa kiasi cha shilingi milioni tatu kutoka kwa Katibu wa Tume ya Utumishu wa Walimu Tanzania (TSC), Mwl. Paulina Mbena Nkwama kwa ajili ya waathirika wa maafa ya mafuriko katika Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara.

Dkt. Yonazi amepokea msaada huo ofisini kwake Jijini Dodoma Ijumaa tarehe 05 Januari, 2024.

25/12/2023
Want your business to be the top-listed Government Service in Dodoma?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Telephone

Address


Mtendeni
Dodoma

Opening Hours

Monday 09:00 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30