Mbeya Zonal Referral Hospital

Mbeya Zonal Referral Hospital

Share

Ukurasa rasmi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

Photos from Mbeya Zonal Referral Hospital's post 13/05/2026

WAUGUZI WA MZRH WAWAKILISHA VYEMA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) imeshiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Arusha, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha AICC.

Wataalamu hawa(Wauguzi) wamewakilisha vyema taasisi pamoja na wenzao kutoka sehem mbalimbali Tanzania katika kilele cha maadhimisho hayo ya tarehe 12 Mei yenye kauli mbiu “Wauguzi Wetu, Mustakabali Wetu: Wauguzi Waliowezeshwa Huokoa Maisha.”

Photos from Mbeya Zonal Referral Hospital's post 13/05/2026

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa akipongezwa na Waheshimiwa Wabunge Mei 12, 2026 bungeni jijini Dodoma baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27, hatua inayolenga kuendelea kuimarisha huduma za afya nchini

11/05/2026

WIZARA YA AFYA YAOMBA KUIDHINISHIWA BAJETI TRIL. 1.8 MWAKA 2026/27, FUNGU 52

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa , ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha kiasi cha Shilingi trilioni 1.8 kwa ajili ya Matumizi ya Wizara hiyo katika mwaka wa fedha 2026/27 Fungu 52.

Mheshimiwa Mchengerwa ameyasema hayo leo Mei 11, 2026 Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi Trilioni 1.148 ambazo ni sawa na asilimia 64 ya bajeti iliyotengwa zinaombwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, amesema kuwa kati fedha hizo, fedha za ndani ya nchi ni shililingi Bilioni 789.45 na kiasi cha shilingi Bilioni 358.56 zinatoka kwa washirika wa maendeleo.

Mhe.Mchengerwa ameliambia Bunge kuwa, Wizara ya Afya imepanga kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 652.236 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambayo ni sawa na asilimia 36 ya bajeti iliyotengwa. Amefafanua kuwa kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi Bilioni 516, 323 ni kwa ajili ya mishahara ya Watumishi wa Afya na kiasi cha shilingi Bilioni 135, 913 zitatumika kwa ajili ya matumizi mengineyo

“Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali Watanzania na kuiwezesha Wizara ya Afya kupatiwa fedha nyingi katika miaka mitano iliyopita ambapo Nchi yetu imeendelea kuwa miongoni mwa nchi chache afrika zinazotoa matibabu kwa gharama nafu”amesema Mchengerwa.

Mwisho, Mhe. Mohamed Mchengerwa Waziri wa Afya ameliomba Bunge kuidhinisha kiasi cha jumla ya shilingi Trilioni 1.8 katika mwaka wa fedha 2026/27,amesema kupatika kwa bajeti hiyo kutasaidia kutekeleza shughuli mbalimbali zilizopangwa ikiwemo vipaumbele vyote 11 ambavyo vimelenga kuiweka Tanzania kuwa mfano kwa utoaji bora wa huduma za afya kwa Wananchi Barani Afrika

11/05/2026
11/05/2026

MCHENGERWA KUWASILISHA BAJETI YA WIZARA YA AFYA LEO BUNGENI.

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, leo tarehe 11,Mei,2026 anatarajiwa kuwasilisha bajeti ya Wizara ya Afya bungeni, akieleza vipaumbele vya Serikali katika kuimarisha sekta ya afya kwa mwaka wa fedha ujao.
Katika hotuba hiyo, Serikali inatarajiwa kueleza hatua mbalimbali za kuboresha huduma za afya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kutolea huduma za afya nchini.

Aidha, hatua za utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote zinapewa kupewa kipaumbele na mafanikio ya namba 199, inayotumika kuzungumza na wananchi kuhusu masuala ya afya na huduma mbalimbali na Mpango Mkakati wa Kampeni ya “Jua Namba zako”katika kukabiliana na Magonjwa Yasiyoambukiza pamoja Kampeni ya “Ubongo Hauna Spea,Vaa Helmet na mambo mengine lukuki katika uboreshaji wa Huduma za Afya.

Je, ni kiasi gani Wizara itaidhinishiwa na Bunge katika kufanikisha vipaumbele vyake muhimu ikiwemo eneo la Kinga, Tiba?

Usikose kufuatilia Mubashara kupitia TBC, Crown Media, Uhondo TV, Mzawa TV,Bunge TV na vyombo mbalimbali vya Habari.

10/05/2026

10/05/2026

BungeLaTanzania AfyaBora

10/05/2026

Tunajali Afya yako. Endelea kuwa nasi

Photos from Mbeya Zonal Referral Hospital's post 01/05/2026

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAWATUNUKU VYETI NA ZAWADI WATUMISHI HODARI KATIKA MAADHIMISHO YA MEI MOSI.

Katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kwa mwaka 2026, Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya (MZRH) imewatunuku vyeti na zawadi wafanyakazi wake waliofanya vizuri zaidi katika nyanja mbalimbali za utoaji huduma za afya.

Hafla hiyo fupi na ya kusisimua imefanyika leo katika ukumbi wa hospitali hiyo, ikilenga kutambua mchango wa wafanyakazi hodari ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma bora na za haraka.

Akizungumza wakati wa kutoa vyeti hivyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Dkt. Lazaro Mboma, amewapongeza watumishi hao na kuwataka waendelee kuwa mfano wa kuigwa kwa wenzao.

“Tuzo hizi ni chachu ya kuongeza juhudi. Tunatambua utumishi wenu uliotukuka na tunatarajia kuona mabadiliko makubwa zaidi katika utendaji kazi ili kuifikia azma ya serikali ya kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini,” alisema Dkt. Mboma.

Hafla hiyo ilipambwa na uwepo wa viongozi waandamizi wa hospitali pamoja na wageni waalikwa kutoka Chama cha Madaktari na Wafamasia (TMDPWU), ambao walitoa neno la hamasa kwa watumishi hao, wakisisitiza umuhimu wa kulinda haki na maslahi ya mfanyakazi sambamba na kutoa huduma ya kitaalamu.

Maadhimisho haya ya Mei Mosi 2026 yanakuja wakati ambapo kitaifa yanafanyika mkoani Njombe,

yakiongozwa na kauli mbiu isemayo: “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.”

Watumishi waliotunukiwa vyeti hivyo wameshukuru Uongozi wa hospitali kwa kutambua mchango wao na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu ili kutimiza malengo ya Dira ya Taifa ya mwaka 2050

Want your business to be the top-listed Government Service in Mbeya?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address


Hospital Street
Mbeya