26/05/2026
TFS-Tree seed Production
Tree Seed Production station (TSPS) ni kituo chini ya Wakala wa Huduma za Misitu
26/05/2026
TFS YATOA MICHE 500, YAONGOZA MAPAMBANO YA UHIFADHI BWAWA LA MINDU
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
MOROGORO — Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kupitia Kituo cha Uzalishaji Mbegu za Miti Morogoro, umetoa miche 500 ya miti ya midodoma na kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti katika hifadhi ya chanzo cha maji cha Bwawa la Mindu, ikiwa ni juhudi za kulinda usalama wa maji kwa wakazi wa Manispaa ya Morogoro na maeneo jirani.
Zoezi hilo la pamoja limewakutanisha watumishi wa umma, wastaafu kutoka taasisi mbalimbali pamoja na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), likiwa na lengo la kurejesha na kuhifadhi vyanzo vya maji vinavyotegemewa na zaidi ya wakazi 500,000.
Akizungumza kwa niaba ya Mhifadhi Mkuu wa Kituo cha Uzalishaji Mbegu za Miti Morogoro, Mhifadhi Mwandamizi (SCO) Helman Ndanzi amesema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa TFS katika kuimarisha uhifadhi wa mazingira, hususan katika maeneo nyeti ya vyanzo vya maji.
Amesisitiza kuwa uhifadhi wa mazingira haupaswi kuachwa kwa taasisi moja pekee bali unahitaji ushirikiano wa wadau wote, akibainisha kuwa TFS itaendelea kusambaza miche bora na kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha juhudi hizo zinakuwa endelevu.
Kwa upande wake, Meneja wa Mazingira na Usafi wa Mazingira kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA), Mhandisi Hafidhi Lacha amesema zoezi hilo linaendana na maadhimisho ya Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, akieleza kuwa upandaji miti ni nguzo muhimu katika kulinda vyanzo vya maji.
“Uwepo wa miti katika maeneo ya vyanzo vya maji unasaidia kuhifadhi unyevunyevu wa ardhi, kuzuia mmomonyoko na kuhakikisha upatikanaji wa maji unaendelea kuwa wa uhakika kwa wananchi,” amesema.
Naye Diwani wa Viti Maalum (CCM) wa Kata ya Maghorofani, Immaculate Mhagama ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wauguzi Wastaafu, ametoa wito kwa jamii na makundi mbalimbali kushiriki kikamilifu katika kampeni za upandaji na utunzaji wa miti ili kulinda mazingira kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Amesema ushiriki wa wananchi ni nguzo muhimu katika kufanikisha juhudi za uhifadhi na kwamba kila mmoja ana wajibu wa kutunza miti inayopandwa ili kuhakikisha inaleta matokeo chanya yaliyokusudiwa.
Zoezi hilo linaakisi dhamira ya Serikali kupitia TFS na wadau mbalimbali katika kuhakikisha rasilimali za misitu na maji zinalindwa kwa manufaa ya maendeleo endelevu ya taifa.
TFS YASHIRIKI UZINDUZI MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA MOROGORO
Na Mwandishi Wetu, Morogoro
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia Kituo cha Uzalishaji wa Mbegu za Miti, wameshiriki uzinduzi wa mradi wa kuhifadhi mazingira unaotekelezwa na Shirika la UECO – Unganisha Environmental Conservation kwa kushirikiana na mradi wa Imarika chini ya Mtandao wa PELUM Tanzania.
Uzinduzi huo umefanyika tarehe 17 Aprili 2026 katika Kata ya Mkundi, Manispaa ya Morogoro, ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini, Mheshimiwa M***a Kilakala.
Katika uzinduzi huo, jumla ya mizinga 50 ya kisasa iligawiwa kwa vikundi vya vijana na wanawake kutoka mitaa inayozunguka Mlima wa Mguruwandege ambayo ni Mawasiliano, Kilongo, Kilongo B na Mguruwandege, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuwawezesha wananchi kiuchumi sambamba na kuhifadhi mazingira.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mheshimiwa Kilakala alisisitiza umuhimu wa jamii kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi wa mazingira kwa kutumia mbinu endelevu k**a ufugaji nyuki na upandaji miti, ambazo huchangia kulinda vyanzo vya maji na bioanuwai huku zikitoa kipato kwa wananchi.
Akimwakilisha Mhifadhi Mkuu wa Kituo cha Uzalishaji Mbegu za Miti, Mhifadhi Herman Ndazi alisema TFS itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za miti na kuhamasisha upandaji miti katika maeneo ya hifadhi na nje ya hifadhi ili kukabiliana na changamoto za uharibifu wa mazingira.
Aliongeza kuwa ushirikiano kati ya serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na jamii ni nguzo muhimu katika kufanikisha juhudi za uhifadhi wa misitu na mazingira kwa ujumla.
Mradi huo unalenga kuimarisha uhifadhi wa Mlima wa Mguruwandege kwa kuwajengea uwezo wananchi katika shughuli mbadala za kiuchumi ambazo haziharibu mazingira, hivyo kuchangia maendeleo endelevu ya jamii zinazouzunguka mlima huo.
26/01/2026
Usikose kupanda mti.
16/12/2025
Pongezi
16/12/2025
Kumekucha
29/10/2025
Ni Leo
01/10/2025
Wasiliana nasi
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Telephone
Website
Address
Kihonda
Morogoro
373
Opening Hours
| Monday | 07:30 - 17:30 |
| Tuesday | 07:30 - 17:30 |
| Wednesday | 07:30 - 17:30 |
| Thursday | 07:30 - 17:30 |
| Friday | 07:30 - 17:30 |
| Saturday | 08:00 - 12:00 |
| Sunday | 09:00 - 12:00 |

28/09/2025
28/09/2025